Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)

Kuhusu Sisi

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi

Historia

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) ulianzishwa rasmi mwaka 1978, ukiwa ni muunganiko wa Afro-Shirazi Party Youth League (ASP-YL) ya Zanzibar na TANU Youth League (TYL) ya Tanganyika. Tangu kuanzishwa kwake, umekuwa chombo kikuu cha Chama katika kuandaa na kuwalea vijana kuwa viongozi na raia wema.

Kwa zaidi ya miaka 40 sasa, UVCCM imekuwa kiungo muhimu katika kuhakikisha kwamba sauti ya vijana inasikika katika mchakato wa kisiasa na maendeleo ya nchi. Umoja huu umejitolea kwa muda mrefu katika kukuza ujasiriamali wa vijana, uwezeshaji wa kiuchumi, na ustawi wa kijamii.

1978

Mwanzilishi

UVCCM ilianzishwa mwaka 1978 baada ya muungano wa ASP-YL na TYL

2025

Wanachama zaidi ya 6M+

Idadi ya wanachama waliosajiliwa kwa sasa

Imani

Tunaamini kwamba binadamu wote ni sawa, na kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake. Imani yetu inajikita katika kuondoa aina zote za ubaguzi, unyonyaji, na rushwa, na kujenga jamii yenye usawa, haki, na amani.

UVCCM inaamini katika nguvu ya vijana kuleta mabadiliko chanya katika jamii. Tunasisitiza umuhimu wa:

  • Uzalendo na upendo kwa nchi na chama
  • Uwajibikaji na uadilifu katika utendaji kazi
  • Heshima kwa mwenendo wa kisasa wa kidemokrasia
  • Ushirikiano wa kitaifa na kimataifa
  • Maendeleo endelevu yanayolenga maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo

Umoja

Kujenga mazingira ya ushirikiano kati ya vijana

Ubunifu

Kuhimiza ubunifu na ujasiriamali wa vijana

Itikadi

Itikadi ya UVCCM ni Ujamaa na Kujitegemea. Inasisitiza umuhimu wa kujenga uchumi imara unaomilikiwa na wananchi, huku serikali ikiweka mazingira wezeshi. Tunahimiza uzalishaji mali kwa pamoja na mgawanyo sawa wa matunda ya jasho la wwwww

Malengo

UVCCM ina malengo makubwa ya kuhakikisha kwamba vijana wa Tanzania wanashiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi na kuwa viongozi wa kesho. Malengo yetu makuu in pamoja na:

  • Kuwaandaa vijana kuwa wanachama na viongozi waadilifu wa Chama Cha Mapinduzi.
  • Kuelimisha vijana juu ya Itikadi ya Chama na umuhimu wa uzalendo.
  • Kuwa chombo cha kuwaunganisha vijana wote nchini bila kujali tofauti zao.
  • Kuhamasisha na kushiriki katika shughuli za ujenzi wa taifa.
  • Kuhimiza na kukuza mipango ya uwezeshaji wa kiuchumi kwa vijana.
  • Kushirikiana na mashirika ya ndani na nje ya nchi kwa maslahi ya vijana.
  • Kuhakikisha vijana wanashiriki kikamilifu katika mchakato wa kisiasa na maamuzi ya kitaifa.
Ushiriki wa Vijana
85%
Uwezeshaji
72%

Muundo wa Uongozi

Itikadi ya UVCCM ni Ujamaa na Kujitegemea. Inasisitiza umuhimu wa kujenga uchumi imara unaomilikiwa na wananchi, huku serikali ikiweka mazingira wezeshi. Tunahimiza uzalishaji mali kwa pamoja na mgawanyo sawa wa matunda ya jasho

Mwenyekiti
UVCCM Taifa
Makamu
UVCCM Taifa
Katibu Mkuu
UVCCM Taifa