SERIKALI CCM KULETA BOTI MBILI ZA KUSAFIRISHA WAGONJWA MULEBA
15 Oct, 2025
50 Machapisho
ðŸ—“ï¸ Tarehe 15 Oktoba 2025
ðŸ“Muleba-Kagera
Katika kuimarisha huduma za afya kwa wananchi wanaoishi katika visiwa na Maeneo ya Mwambao wa Ziwa Victoria, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza mpango wa serikali wa kuleta boti mbili mpya za kisasa kwa ajili ya kusafirisha wagonjwa katika Halmashauri ya Muleba, Mkoa wa Kagera.
Dkt. Samia amesema hatua hiyo Inalenga kupunguza Vifo vya mama Wajawazito na wagonjwa wanaoshindwa kufika Hospitalini kwa wakati, Sambamba na Kuendeleza jitihada za Awamu ya Sita za kuimarisha huduma za afya hadi katika maeneo ya mbali, Uamuzi huu unaonyesha dhamira ya kweli ya serikali ya CCM kuhakikisha hakuna Mtanzania anayepoteza maisha kwa sababu ya umbali au Ukosefu wa usafiri wa dharura hivyo kuendeleza falsafa ya maendeleo yenye kugusa maisha ya watu Moja kwa Moja.
#oktobatunatiki✅✅✅
#fyuchabilastresi
#tokanitoketukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo