AHSANTE KAGERA KWA MAPOKEZI MAZURI YA ILANI YA CCM
17 Oct, 2025
78 Machapisho
ðŸ“Kagera - Tanzania
ðŸ—“ï¸ Alhamisi16 Oktoba, 2025
Serikali ya Chama Cha Mapinduzi Chini ya Mwenyekiti wake Dkt Samia Suluhu Hassan ameendelea kuinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndani ya mkoa wa Kagera leo na kuahidi ahadi zifuatazo zilizopo kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndani ya mkoa wa Kagera;
AFYA
Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imejipanga kuboresha Huduma ya Afya kwa Nchi nzima kwa kutoa Bima ya Afya kwa watu wote ndani ya nchi itakayopelekea kupunguza vifo ndani ya Nchi.
Pia kwenye Sekta ya Afya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imejipanga kwa siku 100 zijazo za kwanza baada ya Uchaguzi, kuwaajiri wataalam mbalimbali kwenye Sekta hii kwa lengo la kuboresha Sekta ya Afya.
ELIMU
Mgombea wa kiti Cha urais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi yuko Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi Uboreshaji wa Sekta Ya Elimu kwa kufanya ujenzi wa Mabweni kwa Shule za Sekondari, Na kutunisha mifuko Ya Elimu ya juu ili vijana wanaomaliza kidato cha Sita.
UMEME
Serikali ya CCM inaenda kumaliza Changamoto ya umeme kwa kujenga kituo cha kupokea na kupooza umeme ndani ya mkoa Wa Kagera ili kuwa na Umeme wa uhakika ndani ya masaa 24 kwa Mwaka.
#oktobatunatiki
#fyuchabilastresi
#tokanitoketukatiki
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko