Chagueni Viongozi wanaojali amani na maendeleo endelevu ya taifa letu
18 Oct, 2025
49 Machapisho
Zanzibar, 17 Oktoba 2025
Uongozi wa Seneti wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Magharibi, ukiongozwa na Mwenyekiti wake Ndg. Ikram Soraga, umeshiriki mafunzo ya elimu kwa mpiga kura katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Karume (KIST), yakilenga kuwaandaa wanavyuo kushiriki uchaguzi mkuu kwa amani ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025.
Mafunzo hayo yametolewa na maafisa kutoka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), ambapo Mgeni Rasmi, Ndg. Zeyana A. Hamid (Mbunge Mteule wa CCM Viti Maalum UWT – Kundi la Wasomi), amewasihi wanavyuo kudumisha amani, kuendelea kuchagua viongozi wanaohubiri maendeleo, na kuenzi mafanikio makubwa yaliyotekelezwa na Serikali ya CCM hususan katika sekta ya elimu, pamoja na mipango iliyoainishwa kwenye Ilani ya CCM 2025–2030.
Kwa upande wake, Ndg. Ikram Soraga aliwahimiza wanavyuo kuendelea kuwa na imani na Chama Cha Mapinduzi, kujitokeza kwa wingi kupiga kura, na kutokubali kushawishiwa na propaganda zinazolenga kuvuruga amani na umoja wa taifa.
#TokaNitokeTukatiki ✅
#KazinaUtuTunasongaMbele ✅
#ZanzibarMpya ✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo