TAARIFA KUTOKA KWA MHESHIMIWA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
08 Dec, 2025
73 Machapisho
Katika kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Uhuru Kesho, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Waziri Mkuu leo, ametoa agizo maalum kwa wananchi wote wa Tanzania.
Mheshimiwa Rais ameelekeza kuwa KILA MTANZANIA ASHIRIKI maadhimisho ya kesho akiwa nyumbani, kama njia ya kutafakari historia ya taifa, kutambua thamani ya uhuru wetu, na kuenzi misingi ya amani na umoja iliyojengwa kwa miaka mingi.
Hata hivyo, agizo hilo halimhusu mfanyakazi ambaye kazi yake ni ya lazima na haiwezi kusimama, wakiwemo madaktari, wauguzi, askari wa ulinzi na usalama, pamoja na watumishi wanaohitajika kwa dharura au huduma muhimu za moja kwa moja kwa wananchi. Watumishi hao wataendelea kutimiza majukumu yao kama kawaida ili kuhakikisha huduma muhimu hazikatiki.
Serikali imesisitiza kuwa maadhimisho haya yawe ya utulivu, uzalendo na umoja, na wananchi wote wanahimizwa kutumia siku hii kutafakari hatua tulizopiga na kujipanga kuendelea kulijenga taifa letu katika misingi ya maendeleo na mshikamano.
#KazinautuTunasongaMbele
#KeshoHatokiMtu
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo