CCM YAANZA HARAMBEE YA UCHAGUZI: WANANCHI WAIPOKEA KWA MIKONO MIWILI
Chama Cha Mapinduzi (CCM) tumezindua rasmi harambee ya kuchangia kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 na kufanikisha kukusanya Shilingi Bilioni 86.31 katika uzinduzi uliofanyika Agosti 12, 2025, katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Uzinduzi huu umepokelewa kwa shangwe na wananchi, wafanyabiashara, wadau wa maendeleo na wanachama wa CCM, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama, Rais Samia Suluhu Hassan. Katika harambee hiyo, Rais Samia alichangia Sh. Milioni 100, huku Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akichangia Sh. Milioni 50.
Jumla ya fedha taslimu zilizokusanywa ni Sh. Bilioni 56.31, huku Sh. Bilioni 30.2 zikiwa ahadi. Hii ni sehemu ya lengo kubwa la chama kukusanya Sh. Bilioni 100 kwa ajili ya maandalizi ya ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi wa 2025.
Akizungumza baada ya kupokelewa kwa michango hiyo, Rais Samia alisema:
“Kutoa ni moyo siyo utajiri. Michango yenu ndiyo ngao ya ushindi wetu na dhamira ya kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli.â€
Aidha, aliwahimiza wananchi wote kuendelea kushiriki harambee hii, wakiwemo Watanzania waishio nje ya nchi (Diaspora).
👉 Jinsi ya Kuchangia kupitia Simu:
-
Piga:
*150*50*1# -
Ingiza Control Number:
C02025 -
Weka Kiasi cha Mchango
-
Ingiza PIN yako kuthibitisha
Michango hii itaendelea kupokelewa hadi Agosti 27, 2025. Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amewahimiza Watanzania wote wenye mapenzi mema kuendelea kushiriki, akisisitiza kuwa hatua hii ni muhimu katika kuandaa ushindi wa chama kinachobeba matumaini ya wananchi
Habari Zinazohusiana
TRILIONI 2.4 ZA RAIS DKT. SAMIA ZAAMSHA MUITIKIO MKUBWA KWA VIJANA WASOMI DAR ES SALAAM
23 Dec, 2025
Dar es Salaam, 23 Desemba 2025 Maelfu ya vijana wasomi wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar es Salaam wamejitokeza kwa wingi katika Hafla ya Ukaribisho wa Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza, iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC, chini ya Mgeni Rasmi Mwenyekiti wa UVCCM Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Ndg. Mohammed Ali Kawaida (MCC).
ATAKAYECHEZEA AMANI YA TAIFA LETU AWE ADUI YETU SOTE
21 Dec, 2025
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida, ametoa wito kwa vijana wote wa Kitanzania, viongozi na wananchi kwa ujumla kulinda, kutetea na kudumisha amani ya Taifa letu. Amesisitiza kuwa amani ya Tanzania ni tunu muhimu na ya msingi kwa ustawi wa Taifa, akibainisha kuwa yeyote atakayethubutu kuichezea amani hiyo hana nafasi katika jamii na anapaswa kuonekana kuwa adui wa wote.
Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Rais wa Tanzania
14 Dec, 2025
Dar es Salaam | 14 Disemba 2025 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Mheshimiwa Antonio Guterres, ameipongeza Tanzania kwa kuendelea kuwa kielelezo cha amani, mshikamano wa kijamii na utulivu wa kisiasa barani Afrika na duniani, licha ya changamoto zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.