CCM YAANZA HARAMBEE YA UCHAGUZI: WANANCHI WAIPOKEA KWA MIKONO MIWILI
Chama Cha Mapinduzi (CCM) tumezindua rasmi harambee ya kuchangia kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 na kufanikisha kukusanya Shilingi Bilioni 86.31 katika uzinduzi uliofanyika Agosti 12, 2025, katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Uzinduzi huu umepokelewa kwa shangwe na wananchi, wafanyabiashara, wadau wa maendeleo na wanachama wa CCM, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama, Rais Samia Suluhu Hassan. Katika harambee hiyo, Rais Samia alichangia Sh. Milioni 100, huku Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akichangia Sh. Milioni 50.
Jumla ya fedha taslimu zilizokusanywa ni Sh. Bilioni 56.31, huku Sh. Bilioni 30.2 zikiwa ahadi. Hii ni sehemu ya lengo kubwa la chama kukusanya Sh. Bilioni 100 kwa ajili ya maandalizi ya ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi wa 2025.
Akizungumza baada ya kupokelewa kwa michango hiyo, Rais Samia alisema:
“Kutoa ni moyo siyo utajiri. Michango yenu ndiyo ngao ya ushindi wetu na dhamira ya kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli.â€
Aidha, aliwahimiza wananchi wote kuendelea kushiriki harambee hii, wakiwemo Watanzania waishio nje ya nchi (Diaspora).
👉 Jinsi ya Kuchangia kupitia Simu:
-
Piga:
*150*50*1# -
Ingiza Control Number:
C02025 -
Weka Kiasi cha Mchango
-
Ingiza PIN yako kuthibitisha
Michango hii itaendelea kupokelewa hadi Agosti 27, 2025. Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amewahimiza Watanzania wote wenye mapenzi mema kuendelea kushiriki, akisisitiza kuwa hatua hii ni muhimu katika kuandaa ushindi wa chama kinachobeba matumaini ya wananchi
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo