MATEMBEZI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YAANZA RASMI MKOA WA MJINI MAGHARIBI
06 Jan, 2026
242 Machapisho
Matembezi ya kuadhimisha Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yameanza rasmi leo katika Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja, yakihusisha makundi mbalimbali ya vijana, wanachama wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na wananchi, waliokusanyika kuonesha mshikamano, uzalendo na heshima kwa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Matembezi hayo yanafanyika chini ya mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Khalid Mwinyi(MNEC), ambaye anaongoza vijana na wanachama wa chama hicho katika kushiriki shughuli hiyo muhimu ya kitaifa yenye lengo la kuenzi misingi, tunu na mafanikio ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanaendelea kuwa nyenzo muhimu ya kuimarisha umoja wa kitaifa, mshikamano wa vijana na kukuza elimu ya uzalendo, huku yakikumbusha mchango mkubwa wa Mapinduzi katika kujenga Zanzibar ya amani, maendeleo na ustawi wa wananchi wake.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko