ZIARA YA KATIBU MKUU CCM DKT.ASHA -ROSE MIGIRO, KUKUTANA NA MABALOZI WA SHINA WA CCM
07 Jan, 2026
106 Machapisho
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Asha Rose Migiro, ameanza ziara yake ya kikazi katika Mkoa wa Dar es Salaam kwa kukutana na kuzungumza na mabalozi wa mashina ya CCM, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa uongozi wa chama wa kuimarisha utendaji kuanzia ngazi ya chini.
Akizungumza kupitia ukurasa wake rasmi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, Dkt. Migiro ameandika:
“Leo nimeanza ziara yangu katika Mkoa wa Dar es Salaam kukutana na kuzungumza na mabalozi wa shina wa Chama Cha Mapinduzi. Ni ari yangu kujua na kufahamu mipango kazi iliyopo kwenye mashina yetu.”
Kupitia ziara hiyo, Katibu Mkuu huyo analenga kusikiliza kwa karibu hali halisi ya uendeshaji wa shughuli za kichama katika mashina, kufahamu mipango waliyojiwekea mabalozi pamoja na changamoto zinazowakabili katika kukijenga, kukilinda na kukikuza Chama Cha Mapinduzi katika jamii.
Ziara ya Dkt. Asha Rose Migiro katika Mkoa wa Dar es Salaam inaakisi dhamira ya dhati ya uongozi wa CCM ya kushuka chini, kuzungumza moja kwa moja na wanachama na kuimarisha mshikamano wa chama kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa, hatua inayotarajiwa kuongeza ari ya utendaji na uwajibikaji miongoni mwa mabalozi na wanachama wa CCM.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko