MWENYEKITI KAWAIDA AONGOZA MATEMBEZI YA KUADHIMISHA MIAKA 62 YA MAPINDUZI MATUKUFU YA ZANZIBAR, KUSINI PEMBA
09 Jan, 2026
65 Machapisho
Na Mwandishi wetu, Kusini Pemba.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Ndugu Mohammed Ali Kawaida (MCC), leo Ijumaa tarehe 09 Januari, 2026 ameongoza maelfu ya vijana katika Matembezi ya Amani ya kuadhimisha Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yaliyofanyika katika Mkoa wa Kusini Pemba.
Matembezi hayo ya kihistoria yalianzia Bandarini Mkoani, yakapitia maeneo ya Mtuhaliwa, Chanjamjawiri, na kuhitimishwa katika Gombani ya Kale, yakihusisha vijana kutoka makundi mbalimbali wakiwa wamevalia mavazi ya kizalendo ya Chama Cha Mapinduzi, wakiwa na mabango, bendera na nyimbo za kizalendo zilizoakisi historia, mshikamano na dhamira ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Akiongoza matembezi hayo, Mwenyekiti Kawaida ameonesha kwa vitendo nafasi ya vijana katika kulinda, kutetea na kuenzi misingi ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar—Mapinduzi yaliyoasisiwa Januari 12, 1964, yakileta usawa, haki ya kijamii, utu na mamlaka ya wananchi wa Zanzibar.
Baada ya kukamilika kwa matembezi hayo, Mwenyekiti Kawaida anatarajiwa kuzungumza na wanamatembezi, ambapo atatoa ujumbe maalum wa kuhitimisha matembezi hayo, ikiwa ni siku ya mwisho ya matembezi ya maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi katika mikoa ya Pemba. Ujumbe huo unalenga kuwakumbusha vijana wajibu wao wa kihistoria katika kuilinda amani, mshikamano wa kitaifa, na kuendeleza kazi na utu kama msingi wa maendeleo ya Taifa.
Maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanaendelea kuwa chachu ya kuimarisha uzalendo, kuenzi mashujaa wa Mapinduzi, na kuimarisha mshikamano wa Watanzania, hususan vijana, katika kujenga Zanzibar na Tanzania yenye maendeleo, haki na usawa kwa wote.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko