DIWANI LUTFIA AONGOZA WANANCHI KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA
25 Jan, 2026
49 Machapisho
Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa kutoka Mkoa wa Mjini Unguja, ambaye pia ni Diwani wa Wadi ya Kwahani, Ndugu Lutfia Juma Idd, ameongoza wakazi wa wadi hiyo kushiriki zoezi la usafi wa mazingira lililofanyika katika maeneo mbalimbali ya wadi hiyo.
Zoezi hilo lililoshirikisha wananchi wa makundi tofauti limejikita katika kusafisha mitaa, maeneo ya wazi na mazingira yanayozunguka makazi ya wananchi, likiwa na lengo la kuimarisha afya ya jamii, kuzuia magonjwa ya mlipuko na kuendeleza utamaduni wa uwajibikaji wa pamoja katika kulinda mazingira.
Kwa upande wake, Umoja wa Vijana wa CCM chini ya Mwenyekiti wake, Ndugu Mohammed Ali Kawaida (MCC), umeendelea kudhihirisha dhamira ya dhati ya kushiriki moja kwa moja katika shughuli za kijamii zenye kugusa maisha ya wananchi, ikiwemo usafi wa mazingira, uhamasishaji wa uzalendo na kuchochea maendeleo endelevu katika jamii.
UVCCM imeendelea kuwa chachu ya mshikamano wa vijana na wananchi kwa ujumla.
#kazinaututunasongambele
#fyuchabilastresi
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko