KATIBU MKUU WA UVCCM ASHIRIKI DUA MAALUM YA KUMUOMBEA RAIS DKT. SAMIA
26 Jan, 2026
38 Machapisho
Zanzibar | Januari 26, 2026
Katibu Mkuu wa UVCCM na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Ndugu Halid Mwinyi, ameshiriki katika dua maalum ya kumuombea kheri Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa iliyoandaliwa na Afisi Kuu ya UVCCM Zanzibar.
Dua hiyo iliambatana na chakula cha pamoja na watoto yatima 800, tukio lililoonesha upendo na mshikamano kwa jamii. Aidha, dua hiyo ni ishara ya shukrani kwa kiongozi anayejali maendeleo ya Taifa na fursa kwa vijana.
Rais Dkt. Samia amekuwa kiongozi wa mfano, anayejali sana vijana na maendeleo ya Taifa zima, jambo ambalo limechochea mshikamano na matumaini kwa wananchi wote .
Hafla ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Rais ilijaa furaha, mshikamano na matumaini, ikionyesha kwa vitendo jinsi kiongozi anavyopendwa na kuthaminiwa na wananchi wake.
#HappyBirthdayDktSamia
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo