Arusha: Mwenyekiti UVCCM Mkoa Simon Maximilian aongoza Maadhimisho ya Miaka 49 ya CCM
31 Jan, 2026
14 Machapisho
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Arusha, Simon Maximilian, awaongoza vijana wa umoja huo katika maadhimisho ya kuelekea miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakionesha uzalendo kwa kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii na za chama.
Vijana hao wametembelea mashina ya chama katika eneo la Nduruma mkoani Arusha na kusimika bendera za CCM katika nyumba za mabalozi, wakisisitiza nafasi muhimu ya balozi kama kiungo cha msingi kati ya chama na wanachama wa ngazi ya chini.
Akizungumza wakati wa shughuli hizo, Maximilian anasema mabalozi ni nguzo muhimu ya chama kwani wanachama wote huanzia ngazi ya shina, hivyo wanastahili kutambuliwa na kuenziwa.
Mbali na shughuli za kichama, maadhimisho hayo yanaambatana na upandaji miti na ukabidhi wa miche miambili katika Hospitali ya Nduruma, tukio linaloonyesha dhamira ya vijana wa UVCCM kuunga mkono utunzaji wa mazingira na kusaidia jamii. Miche hiyo imekabidhiwa hospitalini kama sehemu ya juhudi za kurejesha na kuimarisha huduma za mazingira.
Maadhimisho haya yanathibitisha jitihada za UVCCM kuendelea kuenzi historia ya chama, kuenzi waanzilishi wake, na kushirikisha vijana katika malengo ya maendeleo ya taifa.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo