Mhe. Muhsin Ussi Ashiriki Ugawaji wa Vifaa vya Usafi Zahanati ya Kitunda Kuelekea Miaka 49 ya CCM
02 Feb, 2026
18 Machapisho
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa (kundi la Vijana) na Mbunge wa Jimbo la Malindi, Mheshimiwa Muhsin Ussi, ameshiriki katika zoezi la kugawa vifaa vya usafi katika Zahanati ya Kitunda, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Zoezi hilo limeandaliwa na Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ilala, kama sehemu ya shughuli za kijamii zinazoakisi dhamira ya chama katika kuwatumikia wananchi na kuimarisha ustawi wa jamii.
Maadhimisho hayo yamehudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Nasra Mohamed, pamoja na Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Hussein Egobano.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko