Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)
UVCCM Tabora Mjini yaongoza Usafi na Uchangiaji wa Damu Zahanati ya Ng'ambo Kuelekea Miaka 49 ya CCM | UVCCM
Habari Nyingine

UVCCM Tabora Mjini yaongoza Usafi na Uchangiaji wa Damu Zahanati ya Ng'ambo Kuelekea Miaka 49 ya CCM

02 Feb, 2026 Admin User 41 views min read
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Tabora Mjini, Ndugu Shabani Hussein Nassro, ameongoza vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tabora Mjini katika zoezi la usafi wa mazingira katika Zahanati ya Ng'ambo, pamoja na kushiriki zoezi la kujitolea damu salama, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa CCM.
Shughuli hiyo imeakisi mshikamano, uzalendo na dhamira ya vijana wa UVCCM katika kuchangia maendeleo ya jamii na kuboresha ustawi wa wananchi.
“Tumechagua umoja na amani kwa maendeleo ya taifa letu.”