KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA CCM KIMKOA, WILAYA YA PANGANI
04 Feb, 2026
63 Machapisho
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndugu Halidi Mwinyi, leo anatarajiwa kuongoza sherehe za maadhimisho ya kumbukizi ya miaka 49 tangu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika ngazi ya mkoa, zitakazofanyika Wilaya ya Pangani.
Katibu Mkuu UVCCM, Ndugu Halidi Mwinyi alipokea Bendera za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka kwa Vijana wa CCM Wilaya ya Pangani, waliotekeleza matembezi ya siku saba mfululizo, wakipita katika kata zote 14 za wilaya hiyo, ikiwa ni ishara ya mshikamano, uzalendo na uhai wa chama kuanzia ngazi ya tawi(shina).
Sambamba na hilo, Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa alifungua Mashina ya Wakeleketwa wa Umoja wa Vijana wa CCM katika Kata ya Pangani Mashariki, hatua inayolenga kuimarisha misingi ya chama na kuongeza nguvu ya uhamasishaji kwa vijana na wanachama kwa ujumla.
Aidha, alisisitiza kuwa chama ni wanachama na mtaji mkubwa wa chama ni wanachama, Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa alishiriki pia katika zoezi la upandishaji wa Bendera ya CCM kwa Mabalozi wa Mashina katika Kata ya Pangani Mashariki, kama ishara ya kuimarisha uhai wa Chama Cha Mapinduzi kuanzia ngazi ya Shina.
Maadhimisho hayo yalifanyika katika hali ya amani, mshikamano na umoja, yakibeba ujumbe wa kuendelea kulinda amani na kuimarisha maendeleo ya Taifa kupitia mshikamano wa Watanzania.
Maadhimisho ya miaka 49 ya CCM yanaongozwa na kauli mbiu isemayo:-
“TUMECHAGUA UMOJA NA AMANI KWA MAENDELEO YA TAIFA LETU.”
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko