UVCCM
Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)

KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR

09 Feb, 2026 47 Machapisho
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
Kikao hicho kitaanza rasmi kuanzia saa 8:00 mchana, na kinatarajiwa kujadili masuala muhimu ya kiutendaji, kimkakati pamoja na mwelekeo wa jumla wa utekelezaji wa majukumu ya UVCCM kwa kipindi husika.
UVCCM, kama jumuiya yenye dhamana ya kuandaa, kuunganisha na kuongoza vijana wa Kitanzania kisiasa, imeendelea kusimamia shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya uongozi wa vikao, uwajibikaji na maamuzi ya pamoja