KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
47 Machapisho
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
Kikao hicho kitaanza rasmi kuanzia saa 8:00 mchana, na kinatarajiwa kujadili masuala muhimu ya kiutendaji, kimkakati pamoja na mwelekeo wa jumla wa utekelezaji wa majukumu ya UVCCM kwa kipindi husika.
UVCCM, kama jumuiya yenye dhamana ya kuandaa, kuunganisha na kuongoza vijana wa Kitanzania kisiasa, imeendelea kusimamia shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya uongozi wa vikao, uwajibikaji na maamuzi ya pamoja
Habari Zinazohusiana
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA CCM KIMKOA, WILAYA YA PANGANI
04 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndugu Halidi Mwinyi, leo anatarajiwa kuongoza sherehe za maadhimisho ya kumbukizi ya miaka 49 tangu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika ngazi ya mkoa, zitakazofanyika Wilaya ya Pangani.