Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)
KATIBU UVCCM (W) SONGEA MJINI AENDELEA NA ZIARA YA KITENDAJI KATA ZA MATEKA NA MAJENGO | UVCCM
Habari za Wilaya

KATIBU UVCCM (W) SONGEA MJINI AENDELEA NA ZIARA YA KITENDAJI KATA ZA MATEKA NA MAJENGO

26 Mar, 2026 Admin User 37 views min read
Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Songea Mjini, Ndugu David J. Mlonga, ameendelea na ziara yake ya kitendaji katika Kata za Mateka na Majengo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha uhai wa Jumuiya na kuongeza ushiriki wa vijana.
Katika ziara hiyo, Katibu Mlonga amekagua shughuli za Jumuiya na kuhamasisha mshikamano miongoni mwa vijana, akisisitiza umuhimu wa kuitumikia UVCCM kwa nguvu zote na kwa uzalendo mkubwa.
Aidha, amewahimiza vijana kujikita katika ubunifu na uanzishaji wa miradi mipya ya kiuchumi katika ngazi za kata na matawi, akibainisha kuwa hatua hiyo itaiwezesha Jumuiya kuwa na nguvu ya kifedha na kuendesha shughuli zake kwa ufanisi bila vikwazo.