KISHINDO CHA DKT.NCHIMBI NYANG'HWALE NI USHINDI TU
05 Sep, 2025
116 Machapisho
Maelfu ya wananchi wa Nyang’hwale, mkoani Geita leo Septemba 5, 2025 wamejitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Saba Saba kumpokea na kumsikiliza Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiendelea na mikutano ya kampeni za CCM. Mapokezi hayo yameonesha imani kubwa ya wananchi kwa CCM na kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Urais wa CCM.
Akihutubia wananchi, Dkt. Nchimbi amewataka kujiandaa kwa Oktoba 29 kuhakikisha kura zote za kishindo ni za CCM. Amebainisha kuwa chama hicho kimeendelea kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli kupitia miradi ya afya, elimu, kilimo, viwanda na nishati, hivyo wananchi hawana sababu ya kuyumba. Pia aliwanadi wagombea wa ubunge na udiwani akiwemo Hallen Nassor Amar (Buldoza), Mgombea Ubunge wa Jimbo la Nyang’hwale.
Wananchi wa Nyang’hwale walilipuka kwa shangwe na hamasa kubwa wakiahidi kwa sauti moja kuwa hawatapoteza kura hata moja nje ya CCM. Nyang’hwale waapa kuwa 29 Oktoba ni ushindi wa kishindo kwa Dkt. Samia na ubunge CCM na kwa madiwani wa CCM.
#OktobatunatikiFyuchaBilaStresi
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazimaZoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo