ðŸ“VIJANA WAZANZIBAR WAFUNGULIWA MILANGO YA AJIRA ZA KIMATAIFA
19 Sep, 2025
56 Machapisho
â°Ijumaa Tar,19/09/2025
🔛 Zanzibar-Tanzania
Ilani ya CCM 2025–2030 inaleta matumaini mapya kwa vijana wa Zanzibar kupitia mpango Kabambe wa Ajira Kupitia ushirikiano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Wizara ya Mambo ya Nje, mikakati madhubuti imewekwa kuhakikisha vijana wanapata nafasi za ajira ndani na nje ya nchi.
CCM imejipanga kwa vitendo kwa kuendeleza mikataba ya ajira baina ya Tanzania na Mataifa mbalimbali duniani Hatua hii inalenga kuongeza fursa za ajira zenye Staha, kuimarisha ujuzi wa vijana na kupanua upeo wa kipato kwa familia nyingi za Kitanzania, hasa vijana Wanaohitimu elimu ya juu na mafunzo ya ufundi.
Kwa dira hii, vijana wa Zanzibar hawatabaki nyuma tena Ajira za kimataifa zitakuwa chachu ya maendeleo, zikijenga kizazi chenye matumaini, heshima na uwezo wa kushindana katika Soko la dunia, Ni wakati wa kuamini, kushirikiana na kutekeleza kwa vitendo falsafa ya Oktoba Tunatiki, Kijani Tumetulia, Fyucha Bila Stresi.
#KaziNaUtuTunasongaMbele
#OktobaTunatiki
#FyuchaBilaStresi
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko