WANAVYUO CHAGUA CCM, CHAGUA SAMIA,SAMIA ASHINDE KWA KISHINDO
22 Sep, 2025
14 Machapisho
Mkuu wa idara ya uhusiano ya Kimataifa vyuo na vyuo Vikuu UVCCM Taifa *Ndg Emanuel Martine* Leo tarehe 22/09/2025 amekutana na kuzungumza na Timu ya ushindi ya vijana wanavyuo wa vyuo vya kati na vyuo vikuu, viongozi mbalimbali na walezi wa matawi ya vyuo na vyuo vikuu katika mkoa wa Dar es salaam wanaoendelea kuzisaka kura za *Dkt Samia Suluhu Hassan* mgombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM na Mgombea mwenza wake *Balozi Dkt Emmanuel John Nchimbi,* wabunge na Madiwani wa CCM.
Ndg Emanuel Martine amewasisitiza wanavyuo kuzitafuta kura za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan mtu kwa mtu, simu kwa simu, mitaa kwa mitaa, nyumba kwa nyumba, vijiwe kwa Vijiwe na makundi kwa makundi ili kuhakikisha Kura za Dkt Samia Suluhu Hassan zinapatikana kwa wingi, Samia ashinde kwa kushindo *(fact and figure)*
Chama Cha Mapinduzi na wanavyuo ni chanda na pete, wanavyuo wanakipenda Chama Cha Mapinduzi na Chama Cha Mapinduzi kinawapenda wanavyuo kutoka vyuo vya kati na vyuo Vikuu
#WanavyuoChaguaCCMChaguaSAMIA
#FurahayetuSamiawetu2025-2030
#KaziNaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.