WANAVYUO CHAGUA CCM, CHAGUA SAMIA,SAMIA ASHINDE KWA KISHINDO
22 Sep, 2025
59 Machapisho
Mkuu wa idara ya uhusiano ya Kimataifa vyuo na vyuo Vikuu UVCCM Taifa *Ndg Emanuel Martine* Leo tarehe 22/09/2025 amekutana na kuzungumza na Timu ya ushindi ya vijana wanavyuo wa vyuo vya kati na vyuo vikuu, viongozi mbalimbali na walezi wa matawi ya vyuo na vyuo vikuu katika mkoa wa Dar es salaam wanaoendelea kuzisaka kura za *Dkt Samia Suluhu Hassan* mgombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM na Mgombea mwenza wake *Balozi Dkt Emmanuel John Nchimbi,* wabunge na Madiwani wa CCM.
Ndg Emanuel Martine amewasisitiza wanavyuo kuzitafuta kura za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan mtu kwa mtu, simu kwa simu, mitaa kwa mitaa, nyumba kwa nyumba, vijiwe kwa Vijiwe na makundi kwa makundi ili kuhakikisha Kura za Dkt Samia Suluhu Hassan zinapatikana kwa wingi, Samia ashinde kwa kushindo *(fact and figure)*
Chama Cha Mapinduzi na wanavyuo ni chanda na pete, wanavyuo wanakipenda Chama Cha Mapinduzi na Chama Cha Mapinduzi kinawapenda wanavyuo kutoka vyuo vya kati na vyuo Vikuu
#WanavyuoChaguaCCMChaguaSAMIA
#FurahayetuSamiawetu2025-2030
#KaziNaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo