MWINYI AKUTANA NA FIRST TIME VOTERS NANGWA
22 Sep, 2025
55 Machapisho
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM na Mjumbe wa Halmashauri ya CCM Taifa Ndugu Halid Mwinyi amekutana na kuzungumza na Vijana ambao wanatarajia kupiga kura kwa mara ya kwanza (First Time Voters) wa Chuo cha Ufundi cha Nangwa leo tarehe 22 Septemba, 2025 Wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara.
Katika mazungumzo yake, Ndugu Mwinyi amewasihi kuzingatia mafunzo wanayoyapata chuoni hapo kwani ndio msingi pekee utakaowawezesha kukabiliana vyema na uchangamoto za ajira na kujikwamua kiuchumi.
Pamoja na hayo, aliwasisitiza kutambua haki zao za msingi kwani ndio mara yao ya kwanza kushiriki uchaguzi Mkuu hivyo wana wajibu wa kuchagua Viongozi sahihi ambao wanaamini watawawezesha kufikia malengo yao katika jamii inayowazunguka.
Vijana tunasema,
Oktoba ni mwendo wa kutiki ✅ kwa sababu CCM imetuhakikishia fyucha bila stresi.
#OktobaTunatiki✅✅
#FyuchaBilaStresi
#KaziNaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo