MWINYI AKUTANA NA FIRST TIME VOTERS NANGWA
22 Sep, 2025
16 Machapisho
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM na Mjumbe wa Halmashauri ya CCM Taifa Ndugu Halid Mwinyi amekutana na kuzungumza na Vijana ambao wanatarajia kupiga kura kwa mara ya kwanza (First Time Voters) wa Chuo cha Ufundi cha Nangwa leo tarehe 22 Septemba, 2025 Wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara.
Katika mazungumzo yake, Ndugu Mwinyi amewasihi kuzingatia mafunzo wanayoyapata chuoni hapo kwani ndio msingi pekee utakaowawezesha kukabiliana vyema na uchangamoto za ajira na kujikwamua kiuchumi.
Pamoja na hayo, aliwasisitiza kutambua haki zao za msingi kwani ndio mara yao ya kwanza kushiriki uchaguzi Mkuu hivyo wana wajibu wa kuchagua Viongozi sahihi ambao wanaamini watawawezesha kufikia malengo yao katika jamii inayowazunguka.
Vijana tunasema,
Oktoba ni mwendo wa kutiki ✅ kwa sababu CCM imetuhakikishia fyucha bila stresi.
#OktobaTunatiki✅✅
#FyuchaBilaStresi
#KaziNaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.