NYONGEZA YA MSHAHARA KWA WATUMISHI WA UMMA, CHACHU YA UPENDO WA WATUMISHI KWA DKT. SAMIA
28 Sep, 2025
28 Machapisho
Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa, Vyuo na Vyuo Vikuu UVCCM Taifa, Ndg. Emanuel Martine, leo tarehe 28/09/2025 amekutana na walimu makada na wazalendo wa Mkoa wa Iringa akiwa ameambatana na Katibu Msaidizi Mkuu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa, Ndg. Bulugu Magege.
Katika mkutano huo, Ndg. Emanuel Martine amewataka walimu na watumishi wa umma kuendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kumpa kura kwa kishindo sambamba na kuwapigia kura wabunge na madiwani wote wa CCM katika uchaguzi mkuu ujao.
Waalimu makada wazalendo wa Iringa wametoa ahadi ya dhati ya kumpa kura nyingi za kishindo mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakieleza wazi kuwa nyongeza za mshahara na maboresho aliyoyafanya yamegusa moja kwa moja maisha yao na kuboresha ustawi wa watumishi wote wa umma nchini.
Kabla ya kikao hicho, Ndg. Emanuel Martine alishiriki pia katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM Mkoa wa Iringa, chini ya uongozi wa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa, Ndg. Agrey Tonga. Kikao hicho kilijadili kwa kina mikakati ya kuhakikisha ushindi wa kishindo wa CCM na Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkoa mzima wa Iringa kupitia nguvu ya vijana.
Hakika, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni mama mnyenyekevu, mchapa kazi, mwenye upendo wa kweli kwa wananchi wake. Sasa ni wakati wa kila Mtanzania, hususan vijana na walimu, kuhakikisha anapewa kura nyingi tarehe 29/09/2025 ili kuendeleza kazi kubwa na njema alizoanzisha.
#OktobaTunatiki✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazazoteTunawashaKijani
#WanavyuoChaguaCCMChaguaSAMIA
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.