DKT SAMIA AKIONGEA NA WAPIGA KURA WAKE SHINYANGA MJINI
11 Oct, 2025
53 Machapisho
ðŸ—“ï¸ Tarehe 11/10/2025
📠Shinyanga -Tanzania
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daktari Samia Suluhu Hassan, ameendelea na kampeni zake kwa kishindo akiwa Shinyanga Mjini, ambako amezungumza na Maelfu ya wananchi waliokusanyika kumsikiliza, Akiwa jukwaani Dkt. Samia amesisitiza dhamira ya serikali ya awamu ya sita kuendeleza utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo barabara, maji, afya, elimu na nishati ambayo Imeleta Mapinduzi makubwa katika maisha ya wananchi wa Shinyanga.
Amehimiza pia umuhimu wa amani, umoja na mshikamano wa kitaifa kama nguzo kuu ya Maendeleo na Ustawi wa Taifa, Daktari Samia amewataka wananchi waendelee kuiamini CCM kwa vitendo vyake, Wakitambua kuwa Chama hicho kimekuwa chachu ya Maendeleo halisi yanayoonekana kote nchini, huku akiwahimiza wapiga kura wote kutoka, kutikisa na kutiki CCM Tarehe 29 Oktoba 2025 ili Kuendeleza Safari ya Maendeleo Isiyoacha mtu Nyuma.
#OktobaTunatiki ✅ ✅ ✅
#Fyuchabilastress
#TokaNitokeTukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo