UVCCM YASHIRIKI WIKI YA VIJANA KITAIFA MKOANI MBEYA
11 Oct, 2025
61 Machapisho
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umeshiriki katika wiki ya Vijana inayoendelea Jijini Mbeya, ambayo ilizinduliwa rasmi tarehe 10 Oktoba 2025 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (Mb).
Banda la UVCCM linatoa huduma mbalimbali zenye lengo la kuwaelimisha vijana wa Kitanzania kuhusu umuhimu wa kushiriki uchaguzi na kutumia haki yao ya kupiga kura ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025, ikiwemo elimu ya namna sahihi ya kumchagua Mgombea wa Urais kupitia CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kura ya kishindo
Huduma nyingine zinazotolewa ni pamoja na elimu juu ya Mfumo wa Kijani IlaniChatbot (Ilani ya CCM Kidijitali kwa Vijana), usajili wa kielektroniki wa wanachama wa CCM, huduma ya kurejesha namba za kielektroniki kwa waliopoteza, pamoja na kutoa elimu ya uzalendo na umuhimu wa amani ya Taifa letu. Vijana wamejitokeza kwa wingi kutembelea banda la UVCCM, wakipata huduma na elimu ya kisiasa kwa vitendo.
#KazinaUtuTunasongaMbele ✅
#TokaNitokeTukatiki ✅
#OktobaTunatiki ✅
#TunazimazoteTunawashaKijani ✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo