UVCCM YASHIRIKI WIKI YA VIJANA KITAIFA MKOANI MBEYA
11 Oct, 2025
15 Machapisho
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umeshiriki katika wiki ya Vijana inayoendelea Jijini Mbeya, ambayo ilizinduliwa rasmi tarehe 10 Oktoba 2025 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (Mb).
Banda la UVCCM linatoa huduma mbalimbali zenye lengo la kuwaelimisha vijana wa Kitanzania kuhusu umuhimu wa kushiriki uchaguzi na kutumia haki yao ya kupiga kura ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025, ikiwemo elimu ya namna sahihi ya kumchagua Mgombea wa Urais kupitia CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kura ya kishindo
Huduma nyingine zinazotolewa ni pamoja na elimu juu ya Mfumo wa Kijani IlaniChatbot (Ilani ya CCM Kidijitali kwa Vijana), usajili wa kielektroniki wa wanachama wa CCM, huduma ya kurejesha namba za kielektroniki kwa waliopoteza, pamoja na kutoa elimu ya uzalendo na umuhimu wa amani ya Taifa letu. Vijana wamejitokeza kwa wingi kutembelea banda la UVCCM, wakipata huduma na elimu ya kisiasa kwa vitendo.
#KazinaUtuTunasongaMbele ✅
#TokaNitokeTukatiki ✅
#OktobaTunatiki ✅
#TunazimazoteTunawashaKijani ✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.