DKT. SAMIA AKIZUNGUMZA NA WAPIGA KURA WAKE BUKOMBE
12 Oct, 2025
67 Machapisho
ðŸ—“ï¸ Tarehe 12/10/2025
ðŸ“Bukombe-Geita
Akiwa katika Uwanja wa Bukombe mkoani Geita, Dkt. Samia Suluhu Hassan Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amewasisimua Maelfu ya wananchi waliofurika kumsikiliza kwa shauku na Matumaini makubwa.
Katika hotuba yake yenye msukumo wa maendeleo amesisitiza kuwa serikali anayoiongoza itaendelea kuwekeza kwenye miradi mikubwa ya miundombinu, elimu, afya na upatikanaji wa maji safi vijijini na mijini, huku akiahidi kulinda amani, umoja na heshima ya taifa. Dkt. Samia ametoa wito kwa wananchi wa Bukombe na Watanzania wote kwa ujumla kutoka kwa wingi tarehe 29 Oktoba 2025 na kutiki CCM kama ishara ya kuunga mkono kasi ya maendeleo na uongozi wa hekima unaoweka msingi wa Tanzania yenye fursa, utulivu na mafanikio endelevu.
#OktobaTunatiki
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo