MATEMBEZI YA HESHIMA KUELEKEA KWENYE MKUTANO WA KAMPENI ZA UCHAGUZI BUKOMBE
12 Oct, 2025
11 Machapisho
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Ndg. Mohammed Ali Kawaida (MCC) ameongoza matembezi ya maelfu ya vijana wa Bukombe mkoani Geita kuelekea Uwanjani ambapo unafanyika mkutano wa hadhara wa kampeni wa Mgombea wa Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 12 Oktoba 2025.
Ndg. Kawaida ameambatana na Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Bara, Ndg. Mussa Mwakitinya, Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa, Ndg. Jessica Mshama, Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Geita, Ndg. Manjale Magambo na Mgombea wa Ubunge Arusha Mjini, Ndg. Paul Makonda ambapo maelfu hayo ya vijana wamesema kura zao zote ni kwa Dkt. Samia Oktoba 29.
#OktobaTunatiki✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukaTiki✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.