MATEMBEZI YA HESHIMA KUELEKEA KWENYE MKUTANO WA KAMPENI ZA UCHAGUZI BUKOMBE
12 Oct, 2025
62 Machapisho
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Ndg. Mohammed Ali Kawaida (MCC) ameongoza matembezi ya maelfu ya vijana wa Bukombe mkoani Geita kuelekea Uwanjani ambapo unafanyika mkutano wa hadhara wa kampeni wa Mgombea wa Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 12 Oktoba 2025.
Ndg. Kawaida ameambatana na Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Bara, Ndg. Mussa Mwakitinya, Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa, Ndg. Jessica Mshama, Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Geita, Ndg. Manjale Magambo na Mgombea wa Ubunge Arusha Mjini, Ndg. Paul Makonda ambapo maelfu hayo ya vijana wamesema kura zao zote ni kwa Dkt. Samia Oktoba 29.
#OktobaTunatiki✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukaTiki✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo