MKUU WA MKOA WA SONGWE AFURAHISHWA NA UBUNIFU WA UVCCM KUPITIA MFUMO WA “KIJANI ILANI CHATBOT
15 Oct, 2025
70 Machapisho
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Jabiri Omari Makame, ametembelea banda la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) katika Maonesho ya Wiki ya Vijana Kitaifa yaliyotamatika katika Viwanja vya Uhindini Jijini Mbeya leo tarehe 14 Oktoba 2025 na kutoa pongezi kwa ubunifu wa kidijitali uliofanywa na vUVCCM chini ya uongozi bora wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Ndugu Mohamed Ali Kawaida (MCC).
Akizungumza baada ya kutembelea banda hilo, Mheshimiwa Makame ambaye pia aliwahi kuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa (2012–2015) amepongeza mfumo wa kisasa wa “Umoja wa Vijana wa Ilani ya CCM Kijani Ilani Chatbotâ€, akisema ni njia bora na ya ubunifu wa habari na mawasiliano inayowawezesha vijana kujifunza kuhusu utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020–2025 na kujua malengo ya Ilani ijayo ya CCM 2025–2030 kwa urahisi zaidi kupitia teknolojia.
Ameeleza kuwa Kijani Ilani Chatbot ni mfano wa mwelekeo mpya wa UVCCM katika kutumia TEHAMA kama nyenzo ya elimu, ushirikishwaji, na mawasiliano.
Makame ameongeza kuwa: “Msingi wa Mwenge wa Uhuru ni Umoja wa Vijana wa CCM, na ndiyo maana nembo ya UVCCM ina Mwenge wa Uhuru.â€
KAULI MBIU:
💪 NGUVU KAZI YA VIJANA KWA MAENDELEO ENDELEVU
SHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025 KWA AMANI NA UTULIVU
#KazinaUtuTunasongaMbele ✅
#TokaNitokeTukatiki ✅
#OktobaTunatiki ✅
#TunazimazoteTunawashaKijani ✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo