DKT. SAMIA: TUMEMPOTEZA KIONGOZI MAHIRI NA MPENDA AMANI
15 Oct, 2025
43 Machapisho
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mgombea Urais kupitia tiketi ya CCM Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Mheshimiwa Raila Amolo Odinga, akimtaja kuwa kiongozi mahiri, Mwanamajumui wa Afrika, mpenda amani na mtafuta suluhu.
Amesema Raila alikuwa na ushawishi na upendo uliovuka mipaka ya Kenya na kwamba msiba huu sio wa Wakenya pekee, bali pia ni wa Watanzania na Waafrika wote.
“Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninatuma salamu za pole kwa Rais wa Kenya, Mheshimiwa Dkt. William Samoei Ruto, Mama Ida Odinga, watoto, familia, ndugu, jamaa, marafiki na wananchi wote wa Kenya kwa msiba huu,†amesema Rais Dkt. Samia.
Aidha, Rais Samia ameungana na familia ya Odinga kuwaombea faraja, subra na imani katika kipindi hiki kigumu, huku akiomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Mheshimiwa Raila Amolo Odinga mahali pema peponi, Aamiin .
#KazinaUtuTunasongaMbele
#OktobatunatikiFyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki.
#TunazimaZoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo