SERIKALI KUKAMILISHA TAWI LA CHUO KIKUU CHA UDSM KAGERA
16 Oct, 2025
50 Machapisho
ðŸ—“ï¸ Tarehe 16 Oktoba,2025
ðŸ“Bukoba Mjini-Kagera
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM, Ndugu Samia Suluhu Hassan akiwa Bukoba Mjini, Mkoa wa Kagera, amesema kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika elimu ya juu kwa kukamilisha tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kagera hatua itakayokuza fursa za elimu, kuongeza utafiti na kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Ukanda wa ziwa.
Amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya Serikali kuhakikisha elimu bora inapatikana karibu na wananchi wote bila kujali umbali wala hali zao za kiuchumi, Aidha amesisitiza kuwa Uwepo wa chuo hicho Utachochea ajira, ubunifu na Maendeleo Endelevu katika Mkoa wa Kagera.
#oktobatunatiki✅✅✅
#fyuchabilastresi
#tokanitoketukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo