FARIS BURUHANI AHAIMIZA VIJANA WA KAGERA KUSHIRIKI UCHAGUZI NA KUMCHAGUA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
17 Oct, 2025
12 Machapisho
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera, Faris Buruhani, ameeleza kuwa serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeleta mafanikio makubwa kwa vijana, ikiwemo kuinua sekta ya kilimo, maendeleo ya elimu, fursa za ajira na uongozi, pamoja na huduma bora za afya.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Bukoba, Faris aliwahimiza vijana kushiriki uchaguzi wa Oktoba 29, 2025, kwa amani na utulivu, na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na wagombea wa CCM wa ubunge na madiwani.
Faris alimshukuru Rais Samia kwa namna anavyoendelea kuwathamini na kuwapa nafasi vijana katika uongozi wa kitaifa, akibainisha kuwa uongozi wake umeleta matumaini makubwa kwa kizazi kipya cha Watanzania.
Ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Dkt. Samia, bei ya kahawa, zao kuu la biashara mkoani Kagera imepanda kwa kiwango kikubwa, hali iliyowawezesha vijana wengi kuinuka kiuchumi kupitia sekta ya kilimo. Rais Dkt.Samia amekuwa akiwajali na kuwathamini Watanzania wote hasa vijana.
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.