FARIS BURUHANI AHAIMIZA VIJANA WA KAGERA KUSHIRIKI UCHAGUZI NA KUMCHAGUA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
17 Oct, 2025
85 Machapisho
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera, Faris Buruhani, ameeleza kuwa serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeleta mafanikio makubwa kwa vijana, ikiwemo kuinua sekta ya kilimo, maendeleo ya elimu, fursa za ajira na uongozi, pamoja na huduma bora za afya.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Bukoba, Faris aliwahimiza vijana kushiriki uchaguzi wa Oktoba 29, 2025, kwa amani na utulivu, na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na wagombea wa CCM wa ubunge na madiwani.
Faris alimshukuru Rais Samia kwa namna anavyoendelea kuwathamini na kuwapa nafasi vijana katika uongozi wa kitaifa, akibainisha kuwa uongozi wake umeleta matumaini makubwa kwa kizazi kipya cha Watanzania.
Ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Dkt. Samia, bei ya kahawa, zao kuu la biashara mkoani Kagera imepanda kwa kiwango kikubwa, hali iliyowawezesha vijana wengi kuinuka kiuchumi kupitia sekta ya kilimo. Rais Dkt.Samia amekuwa akiwajali na kuwathamini Watanzania wote hasa vijana.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko