DKT SAMIA AWAPONGEZA VIJANA WA HAMASA
17 Oct, 2025
8 Machapisho
🗓 Alhamisi 16 Oktoba 2025
📍 Bukoba Mjini
Mgombea wa kiti cha Urais kupitia tiketi ya CCM Dkt Samia Suluhu Hassan wakati akihitimisha Ziara yake Mkoani Kagera amefanya mkutano wa hadhara katika jimbo la Bukoba Mjini na kuwashukuru viongozi wa chama, wananchi vijana wa hamasa na makundi yote kwa ujumla kwa mapokezi na ushiriki wao mzuri wa mikutano yake ndani ya mkoa huo.
Aidha kwa upekee ametoa pongezi za dhati kwa makundi ya hamasa kwa kuchangamsha mikutano na kuwafanya watu kufurahia na kusikiliza kwa umakini yote mazuri ya Chama cha mapinduzi, pongezi hizi ni wazi kabisa zinaonesha uimara na maandalizi mazuri ya Jumuiya ya UVCCM Taifa chini ya Ndugu Mohammed Ali Kawaida (MCC) ambae amekuwa mstari wa mbele wakati wote kwa vijana.
#OktobaTunatiki ✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.