SERIKALI YA CCM KUJENGA UZIO WA MAFURIKO RUFIJI
20 Oct, 2025
73 Machapisho
Rufiji-Pwani,Katika mkutano uliojaa hamasa na matumaini mapya kwa wananchi wa Rufiji, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametangaza mpango kabambe wa serikali wa kujenga uzio maalum wa kuzuia mafuriko katika bonde la Rufiji.
Amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya CCM kuhakikisha wananchi wanaishi kwa usalama na shughuli za kilimo, biashara na makazi haziathiriwi tena na maafa ya mvua kubwa, Dkt. Samia amesisitiza kuwa serikali itasimamia utekelezaji wake kwa vitendo ili kulinda maisha ya Watanzania na kuendeleza kasi ya maendeleo endelevu nchini.
#oktobatunatiki✅✅✅
#fyuchabilastresi
#tokanitoketukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo