DKT SAMIA TUNA KAMPUNI ZAIDI YA NNE (4) ZA USAFIRI MWENDOKASI DAR
22 Oct, 2025
65 Machapisho
Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kwa tiketi ya CCM *Dkt. Samia Suluhu Hassan,* ameonyesha dhamira thabiti ya kuboresha huduma za usafiri jijini Dar es Salaam kupitia mfumo wa Usafiri wa Mabasi ya Mwendokasi (UDART). Hivi karibuni, Serikali inaendelea kufanya mazungumzo na kampuni nne kuendesha huduma za mabasi katika njia zinazofikia vituo vya mwisho vya mwendokasi
Uwepo wa kampuni hizi unatarajiwa kuongeza ufanisi na ushindani chanya katika sekta ya usafiri wa umma, kupunguza msongamano wa abiria katika vituo, na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, za haraka na zenye bei nafuu. Hatua hii pia inafungua fursa za ajira kwa vijana, kuongeza mapato ya Serikali kupitia kodi, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa kuboresha mtiririko wa watu na biashara katika jiji la Dar es Salaam.
#OktobaTunatiki✅✅✅
#TokaNitokeTukatiki✅
#FyuchaBilaStresi
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo