DKT SAMIA TUNA KAMPUNI ZAIDI YA NNE (4) ZA USAFIRI MWENDOKASI DAR
22 Oct, 2025
5 Machapisho
Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kwa tiketi ya CCM *Dkt. Samia Suluhu Hassan,* ameonyesha dhamira thabiti ya kuboresha huduma za usafiri jijini Dar es Salaam kupitia mfumo wa Usafiri wa Mabasi ya Mwendokasi (UDART). Hivi karibuni, Serikali inaendelea kufanya mazungumzo na kampuni nne kuendesha huduma za mabasi katika njia zinazofikia vituo vya mwisho vya mwendokasi
Uwepo wa kampuni hizi unatarajiwa kuongeza ufanisi na ushindani chanya katika sekta ya usafiri wa umma, kupunguza msongamano wa abiria katika vituo, na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, za haraka na zenye bei nafuu. Hatua hii pia inafungua fursa za ajira kwa vijana, kuongeza mapato ya Serikali kupitia kodi, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa kuboresha mtiririko wa watu na biashara katika jiji la Dar es Salaam.
#OktobaTunatiki✅✅✅
#TokaNitokeTukatiki✅
#FyuchaBilaStresi
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.