MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
79 Machapisho
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025
Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.
Akiwa katika mkutano wa uhamasishaji wa wananchi kujitokeza kupiga kura, Ndg. Martine alieleza kuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa kinara katika kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati nchini, kupitia ongezeko kubwa la mikopo isiyo na riba kutoka Halmashauri kwa makundi maalum ya kijamii:
Wanawake: TZS Bilioni 99
Vijana: TZS Bilioni 96
Walemavu: TZS Bilioni 45.
“Mikopo hii ni ushahidi tosha kwamba Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan anatekeleza kwa vitendo dhamira ya kuwawezesha Watanzania kiuchumi. Hivyo tarehe 29 Oktoba, ni lazima kila kijana na kila mfanyabiashara atoke na kitambulisho chake cha mpiga kura kwenda kutiki NDIYO kwa CCM,†alisema Martine.
Aliwasisitiza wananchi wote kubeba vitambulisho vya wapiga kura, kujitokeza mapema vituoni na kuhakikisha wanampigia kura Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya Urais, pamoja na wagombea wa Ubunge na Udiwani kutoka CCM, ili kuendeleza kasi ya maendeleo na ustawi wa Taifa.
#TokaNitokeTukatiki ✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazimaZoteTunawashaKijani
#FyuchaBilaStresi
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko