MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
12 Machapisho
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025
Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.
Akiwa katika mkutano wa uhamasishaji wa wananchi kujitokeza kupiga kura, Ndg. Martine alieleza kuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa kinara katika kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati nchini, kupitia ongezeko kubwa la mikopo isiyo na riba kutoka Halmashauri kwa makundi maalum ya kijamii:
Wanawake: TZS Bilioni 99
Vijana: TZS Bilioni 96
Walemavu: TZS Bilioni 45.
“Mikopo hii ni ushahidi tosha kwamba Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan anatekeleza kwa vitendo dhamira ya kuwawezesha Watanzania kiuchumi. Hivyo tarehe 29 Oktoba, ni lazima kila kijana na kila mfanyabiashara atoke na kitambulisho chake cha mpiga kura kwenda kutiki NDIYO kwa CCM,” alisema Martine.
Aliwasisitiza wananchi wote kubeba vitambulisho vya wapiga kura, kujitokeza mapema vituoni na kuhakikisha wanampigia kura Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya Urais, pamoja na wagombea wa Ubunge na Udiwani kutoka CCM, ili kuendeleza kasi ya maendeleo na ustawi wa Taifa.
#TokaNitokeTukatiki ✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazimaZoteTunawashaKijani
#FyuchaBilaStresi
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
SERIKALI KUWAPATIA FURSA WATU WENYE MAHITAJI MAALUMU
23 Oct, 2025
Temeke Dar es salaam Mgombea wa kiti cha Urais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dkt Samia Suluhu Hassan leo akiwa Temeke ameeleza kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imewapa Fursa mabalimbali watu wenye mahitaji Maalum na kuwapa vipaumbele pia kwenye Ajira.