WANAVYUO LINDENI AMANI NA UTULIVU MTAKAPOFUNGUA VYUO, KILA MMOJA ANA WAJIBU WA KULINDA AMANI NA UTULIVU NCHINI TANZANIA
12 Nov, 2025
50 Machapisho
Ndg. Emanuel Martine
Upanga, Dar es Salaam
Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa, Vyuo na Vyuo Vikuu UVCCM Taifa, Ndg. Emanuel Martine, leo tarehe 12.11.2025 amefanya mazungumzo na wanavyuo mbalimbali waliofika kumtembelea katika ofisi za Upanga, jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo hayo, Ndg. Martine amewaomba wanavyuo hao na wanavyuo wote nchini kuhakikisha kila mmoja katika chuo chake analinda amani na utulivu vyuoni na nchini kwa ujumla, watakapofungua vyuo, na kusoma kwa bidii kwa manufaa ya Tanzania.
Martine amesema, “Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kutekeleza utoaji wa mikopo kwa wanavyuo wa vyuo vya kati na vyuo vikuu. Kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na taasisi zote zilizopo chini yake, Serikali imejipanga vyema kuwahudumia wanavyuo katika vyuo vyao, zikiwemo menejimenti za vyuo.â€
Ameongeza kuwa, “Serikali imetenga Bilioni 916.5 kugharamia masomo ya wanavyuo wa vyuo vya kati, vyuo vikuu, na wale wa ufadhili wa Samia Scholarship pamoja na Samia Extended Program. Aidha, Serikali inaendelea kutoa elimu bila ada kwa kidato cha tano na cha sita. Hivyo, wanavyuo wote wanapaswa kuwa watulivu nyakati zote kwani Serikali imefanya mageuzi makubwa katika sekta ya elimu, ikiwemo ongezeko maradufu la bajeti ya mikopo kutoka Bilioni 464 mwaka 2020/2021 hadi Bilioni 916.5 mwaka 2025/2026.â€
“Ndoto, maono na mawazo tuliyonayo kama vijana yatatimia na kufanikiwa endapo kuna ustawi wa amani katika nchi yetu. Amani hii tuitunze kama mboni ya jicho kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu na vizazi vyetu.â€
“Amani ya Tanzania tunapaswa kuilinda sote kwa pamoja. Amani ni msingi wa maendeleo ya taifa letu. Wanavyuo, lindeni amani na utulivu vyuoni mtakapofungua vyuo.â€
#WanavyuoLindeniAmaniNaUtulivuVyuoni
#KaziNaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko