SERIKALI CHINI YA RAIS DKT.SAMIA KUANZISHA WIZARA KAMILI YA VIJANA
14 Nov, 2025
79 Machapisho
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali yake anayoiongoza ya awamu ya sita imedhamiria kuanzisha Wizara kamili itakayoshughulikia masuala yote yanayohusiana na Vijana.
Akizungumza wakati akihutubia katika ufunguzi wa Bunge la 13 la Tanzania leo tarehe 14 Novemba 2025 Jijini Dodoma, Rais Dkt. Samia amesema anatarajia kuwa na Washauri wa Rais watakaomshauri kuhusu mambo ya Vijana ikiwemo changamoto zao.
Mimi na wenzangu katika Serikali tumefikiria kuwa na Wizara kamili itakayoshughulikia mambo ya Vijana
Tumeamua kuwa na Wizara kamili badala ya kuwa na Idara iliyo na mambo mengi
Vilevile nafikiria kuwa na Washauri wa mausala ya Vijana ndani ya Ofisi ya Rais
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko