RAIS SAMIA AWATAKIA HERI WANAFUNZI WANAOHITIMU KIDATO CHA NNE
17 Nov, 2025
80 Machapisho
Rais Dkt. Samia amewatakia heri na baraka wanafunzi 595,816 wa Kidato cha Nne wanaoanza mtihani wa kuhitimu leo tarehe 17 Nov, 2025 katika shule 5,868 nchini.
Amesisitiza kuwa, pamoja na juhudi za Serikali za kujenga miundombinu, shule 305 mpya zinafanya mtihani huu kwa mara ya kwanza mwaka huu 2025 hatua inayothibitisha dhamira ya Serikali ya kupanua fursa za elimu bora kwa watoto wote wa Tanzania.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rais Samia ameandika:-
*"Ninawatakia kila la kheri wanafunzi wote 595,816 wa Kidato cha Nne ambao leo mnaanza mtihani wa kuhitimu elimu ya sekondari katika shule za sekondari 5,868 nchini. Mwenyezi Mungu Mtukufu awajalie utulivu mfanye na mkamilishe vyema hatua hii muhimu kwenye maisha yenu.
*Ninawaombea pia mwendelee kuwa na nidhamu, upendo na bidii katika hatua zinazofuata. Serikali itaendelea kuhakikisha ndoto zenu zinapata nafasi ya kukua na kustawi kwa manufaa yetu sote."
Vijana wote wa Kitanzania tunaungana na Rais wetu Dkt. Samia kuwatakia heri wanafunzi wote wa Tanzania wanaoanza mitihani yao leo. Mafanikio yenu ni fahari ya taifa letu, Mungu awabariki sana 🇹🇿
#KazinaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko