KAWAIDA AHUDHURIA KIKAO MAALUM CHA KAMATI KUU YA CCM
30 Nov, 2025
114 Machapisho
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) na Mjumbe wa Kamati Kuu Ndugu Mohammed Kawaida, ameungana na viongozi wakuu wa Chama cha Mapinduzi katika kikao maalum cha Kamati Kuu ya CCM, kilichoongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kikao hicho, ambacho kimefanyika kisiwani Unguja, ni sehemu muhimu ya mnyororo wa maamuzi ya juu ya chama, kikiwa na lengo la kuimarisha uongozi na mwelekeo wa kisiasa wa CCM na Taifa kiujumla kuelekea utekelezaji wa majukumu yake kwa wananchi.
Katika ajenda zake kuu za leo, Kamati Kuu imepitisha uteuzi wa wagombea wa CCM kwa nafasi za Umeya wa majiji, manispaa, pamoja na wenyeviti wa halmashauri za miji na wilaya, hatua inayotafsiriwa kama mwendelezo wa usimamizi makini katika kuhakikisha wananchi wanapata viongozi bora.
Ushiriki wa Ndugu Kawaida katika kikao hiki unadhihirisha nafasi muhimu ya vijana ndani ya CCM na mchango wake katika kujenga viongozi mahiri na wenye maono ya kuendeleza misingi ya chama na Taifa kiujumla
#KazinaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo