RAIS SAMIA ATWAA TUZO YA KIMATAIFA YA MAJI
Johannesburg, Afrika Kusini – 14 Agosti 2025:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametunukiwa Tuzo ya Kimataifa ya Maji – Presidential Water Changemakers Award 2025 na Global Water Partnership kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika. Hafla ya tuzo hiyo imefanyika katika Mkutano wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Afrika (AU–AIP Africa Water Investment Summit 2025) unaoendelea jijini Johannesburg kuanzia tarehe 13–15 Agosti 2025.
Tuzo hii imetolewa kwa kutambua mchango wa kipekee wa Rais Dkt. Samia katika kuongoza mageuzi makubwa ya sekta ya maji nchini Tanzania, hatua ambazo zimeboresha upatikanaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wa mijini na vijijini.
Chini ya uongozi wake:
- Upatikanaji wa maji vijijini umeongezeka kufikia 79.6%
- Upatikanaji wa maji mijini umefikia 90%
- Miradi mikubwa 1,633 ya usambazaji maji imekamilika
- Vituo vipya vya maji 107,819 vimejengwa
- Zaidi ya wananchi milioni 12 wamenufaika moja kwa moja
- Vijiji 196,160 vimefikiwa na huduma ya maji
Mageuzi haya yameiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia kama mfano wa taifa linalowekeza kwa vitendo katika huduma za kijamii, hususan maji safi na salama.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo