RAIS SAMIA ATWAA TUZO YA KIMATAIFA YA MAJI
Johannesburg, Afrika Kusini – 14 Agosti 2025:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametunukiwa Tuzo ya Kimataifa ya Maji – Presidential Water Changemakers Award 2025 na Global Water Partnership kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika. Hafla ya tuzo hiyo imefanyika katika Mkutano wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Afrika (AU–AIP Africa Water Investment Summit 2025) unaoendelea jijini Johannesburg kuanzia tarehe 13–15 Agosti 2025.
Tuzo hii imetolewa kwa kutambua mchango wa kipekee wa Rais Dkt. Samia katika kuongoza mageuzi makubwa ya sekta ya maji nchini Tanzania, hatua ambazo zimeboresha upatikanaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wa mijini na vijijini.
Chini ya uongozi wake:
- Upatikanaji wa maji vijijini umeongezeka kufikia 79.6%
- Upatikanaji wa maji mijini umefikia 90%
- Miradi mikubwa 1,633 ya usambazaji maji imekamilika
- Vituo vipya vya maji 107,819 vimejengwa
- Zaidi ya wananchi milioni 12 wamenufaika moja kwa moja
- Vijiji 196,160 vimefikiwa na huduma ya maji
Mageuzi haya yameiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia kama mfano wa taifa linalowekeza kwa vitendo katika huduma za kijamii, hususan maji safi na salama.
Habari Zinazohusiana
TRILIONI 2.4 ZA RAIS DKT. SAMIA ZAAMSHA MUITIKIO MKUBWA KWA VIJANA WASOMI DAR ES SALAAM
23 Dec, 2025
Dar es Salaam, 23 Desemba 2025 Maelfu ya vijana wasomi wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar es Salaam wamejitokeza kwa wingi katika Hafla ya Ukaribisho wa Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza, iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC, chini ya Mgeni Rasmi Mwenyekiti wa UVCCM Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Ndg. Mohammed Ali Kawaida (MCC).
ATAKAYECHEZEA AMANI YA TAIFA LETU AWE ADUI YETU SOTE
21 Dec, 2025
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida, ametoa wito kwa vijana wote wa Kitanzania, viongozi na wananchi kwa ujumla kulinda, kutetea na kudumisha amani ya Taifa letu. Amesisitiza kuwa amani ya Tanzania ni tunu muhimu na ya msingi kwa ustawi wa Taifa, akibainisha kuwa yeyote atakayethubutu kuichezea amani hiyo hana nafasi katika jamii na anapaswa kuonekana kuwa adui wa wote.
Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Rais wa Tanzania
14 Dec, 2025
Dar es Salaam | 14 Disemba 2025 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Mheshimiwa Antonio Guterres, ameipongeza Tanzania kwa kuendelea kuwa kielelezo cha amani, mshikamano wa kijamii na utulivu wa kisiasa barani Afrika na duniani, licha ya changamoto zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.