DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUM CHA KAMATI KUU YA CCM
30 Nov, 2025
68 Machapisho
Unguja, 29 Novemba 2025 — Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza Kikao Maalum cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kilichofanyika kisiwani Unguja, Zanzibar.
Kikao hicho muhimu, kilichowakutanisha viongozi wakuu wa chama, kimejadili masuala ya kimkakati yanayohusu utekelezaji wa shughuli za chama katika ngazi mbalimbali za uongozi kwa maendeleo ya Taifa letu la Tanzania.
Miongoni mwa maamuzi makuu yaliyofikiwa, Kamati Kuu imepitisha uteuzi wa wagombea wa CCM kwa nafasi za Umeya wa majiji, manispaa, pamoja na wenyeviti wa halmashauri za miji na wilaya. Uamuzi huo unatajwa kuwa sehemu ya kuweka viongozi bora katika jamii .
Uongozi wa Rais Samia katika kikao hiki unaendelea kudhihirisha msimamo wake thabiti wa kujenga CCM imara, yenye misingi ya uwajibikaji, umoja na ustawi wa wananchi
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo