REUBENS E. SAGAYIKA AAPA RASMI KUWA DIWANI KATA YA KALANGALALA, UVCCM WAMTAKIA HERI
02 Dec, 2025
55 Machapisho
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) unatoa pongezi kwa Reubens E. Sagayika, Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa, kwa kula kiapo cha kuwa Diwani wa Kata ya Kalangalala, Halmashauri ya Wilaya ya Geita.
UVCCM inamtakia heri katika majukumu yake mapya ya kuwatumikia wananchi wa Kalangalala na Watanzania kwa ujumla. Uteuzi na kuapishwa kwake ni uthibitisho wa kuaminika kwa vijana na uwezo wao wa kushika nafasi za uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali.
Imani yake ni imani ya vijana—kuwa vijana wanaweza, vijana wana mchango mkubwa, na vijana ni nguvu ya taifa.
UVCCM tunampongeza sana na tunamtakia utumishi uliotukuka.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo