ATAKAYECHEZEA AMANI YA TAIFA LETU AWE ADUI YETU SOTE
21 Dec, 2025
64 Machapisho
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida, ametoa wito kwa vijana wote wa Kitanzania, viongozi na wananchi kwa ujumla kulinda, kutetea na kudumisha amani ya Taifa letu.
Amesisitiza kuwa amani ya Tanzania ni tunu muhimu na ya msingi kwa ustawi wa Taifa, akibainisha kuwa yeyote atakayethubutu kuichezea amani hiyo hana nafasi katika jamii na anapaswa kuonekana kuwa adui wa wote. Kwa mujibu wake, maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa mazingira ya amani na utulivu.
Ujumbe huo umetolewa tarehe 21 Desemba 2025, mkoani Morogoro, wakati Ndugu Kawaida akizungumza akiwa Mgeni Rasmi katika Semina ya Viongozi Wapya wa Mikoa wa Taasisi ya Mama Aseme. Katika hotuba yake, amesisitiza kuwa jukumu la kulinda na kuimarisha amani ya Taifa ni wajibu wa kila kizazi, hususan vijana na viongozi waliopo madarakani.
Ameongeza kuwa viongozi wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhubiri mshikamano, uzalendo na maadili mema, huku wakikataa na kupinga kwa nguvu zote kauli, vitendo au ajenda zozote zinazoweza kuhatarisha umoja na amani ya Taifa.
Kwa upande wake, Taasisi ya Mama Asemewe imeendelea kuwa sauti imara ya kuelimisha na kuunganisha jamii, sambamba na kueleza ukweli kuhusu kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, hususan katika kulinda amani, kuimarisha demokrasia na kusukuma mbele maendeleo ya wananchi.
#KazinaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko