TRILIONI 2.4 ZA RAIS DKT. SAMIA ZAAMSHA MUITIKIO MKUBWA KWA VIJANA WASOMI DAR ES SALAAM
23 Dec, 2025
57 Machapisho
Dar es Salaam, 23 Desemba 2025
Maelfu ya vijana wasomi wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar es Salaam wamejitokeza kwa wingi katika Hafla ya Ukaribisho wa Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza, iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC, chini ya Mgeni Rasmi Mwenyekiti wa UVCCM Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Ndg. Mohammed Ali Kawaida (MCC).
Hafla hiyo ilijumuisha mapokezi ya heshima, matembezi ya hamasa, na shangwe kubwa kutoka kwa vijana, ikionyesha mshikamano na imani yao kwa uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Katika hotuba yake, Ndg. Kawaida alieleza kwamba Serikali ya Awamu ya Sita imetenga Shilingi Trilioni 2.4 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Sekta ya Elimu kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, ikiwemo ongezeko la Bajeti ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutoka Shilingi Bilioni 464 hadi 787, hatua iliyopokelewa kwa shangwe kubwa na vijana wasomi.
Hafla hiyo imeonyesha wazi kuwa Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaweka elimu na vijana katikati ya maendeleo ya Taifa, ikithibitisha dhamira ya kazi kwa utu na uwekezaji thabiti katika kizazi kijacho.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko