MAELFU WAJITOKEZA KUMSINDIKIZA DKT.SAMIA KUCHUKUA FOMU
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na mgombea mwenza wake Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, wamechukua rasmi fomu za kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Tukio hilo limefanyika , Agosti 9, 2025, katika Ofisi za Tume Huru ya Uchaguzi (INEC) zilizopo Njedengwa, Dodoma.
Mapokezi ya Kishindo
Maelfu ya wananchi, wanachama na wapenzi wa CCM kutoka kila pembe ya Tanzania Bara na Visiwani walijitokeza kwa wingi kwa mapenzi na imani yao kubwa kwa mgombea wao Dkt. Samia. Viwanja vya Makao Makuu ya CCM – Dodoma vilifurika umati wa watu waliobeba mabango zenye jumbe za kuhamasisha ushindi wa chama, huku wakipaza sauti za kumshangilia Rais Samia na mgombea mwenza wake. Wananchi walikuwa wenye furaha kubwa baada ya kuona Dkt.Samia kachukua fomu
Barabara kuu za Dodoma zilijaa wananchi waliokuwa wakisubiri kwa hamu msafara wa wagombea wetu, wengi wakiwa na mabango yenye ujumbe wa kishindo kama vile:“Oktoba Tunakiti!â€â€œSamia ni Tumaini la Watanzaniaâ€â€œDkt Samia Chaguo letu†“Kazi na utu,tunasonga mbele", n.k
Ushuhuda wa mapenzi na imani ya wananchi
Wakati wa tukio hilo, ilidhihirika wazi kuwa watanzania wana imani kubwa na mapenzi ya dhati kwa CCM na mgombea wake Dkt. Samia, ambaye ameendelea kuaminika kutokana na uongozi wake bora wa kidiplomasia na wa maendeleo endelevu.
Kwa upande wake, Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliwashukuru wananchi wote kwa kujitokeza kwa wingi na kusimama bega kwa bega na chama chao. Aliahidi kuendeleza kasi ya maendeleo, mshikamano wa kitaifa na ujenzi wa Taifa lenye matumaini makubwa kwa sasa na baadaye
Habari Zinazohusiana
TRILIONI 2.4 ZA RAIS DKT. SAMIA ZAAMSHA MUITIKIO MKUBWA KWA VIJANA WASOMI DAR ES SALAAM
23 Dec, 2025
Dar es Salaam, 23 Desemba 2025 Maelfu ya vijana wasomi wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar es Salaam wamejitokeza kwa wingi katika Hafla ya Ukaribisho wa Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza, iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC, chini ya Mgeni Rasmi Mwenyekiti wa UVCCM Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Ndg. Mohammed Ali Kawaida (MCC).
ATAKAYECHEZEA AMANI YA TAIFA LETU AWE ADUI YETU SOTE
21 Dec, 2025
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida, ametoa wito kwa vijana wote wa Kitanzania, viongozi na wananchi kwa ujumla kulinda, kutetea na kudumisha amani ya Taifa letu. Amesisitiza kuwa amani ya Tanzania ni tunu muhimu na ya msingi kwa ustawi wa Taifa, akibainisha kuwa yeyote atakayethubutu kuichezea amani hiyo hana nafasi katika jamii na anapaswa kuonekana kuwa adui wa wote.
Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Rais wa Tanzania
14 Dec, 2025
Dar es Salaam | 14 Disemba 2025 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Mheshimiwa Antonio Guterres, ameipongeza Tanzania kwa kuendelea kuwa kielelezo cha amani, mshikamano wa kijamii na utulivu wa kisiasa barani Afrika na duniani, licha ya changamoto zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.