UVCCM yazindua “Kijani Ilani ChatBot
Dar es Salaam – Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Mohammed Kawaida, ameongoza hafla ya uzinduzi wa Kijani Ilani Chat Bot, programu mpya ya kidijitali inayolenga kuongeza hamasa za kisiasa miongoni mwa vijana kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Kawaida alisema kuwa kuimarishwa kwa kampeni za kidijitali ni hatua muhimu ya kuhakikisha vijana wanajitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kupiga kura.
“Teknolojia hii mpya itakuwa nyenzo muhimu kwa vijana kupata taarifa sahihi za Ilani ya Chama, kujua vipaumbele na sera zetu, na kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi,†alisema Kawaida.
Kwa upande wake, Mwenyekiti Mwenza wa UVCCM Taifa, Khalid Mwinyi, alisisitiza umuhimu wa chat bot hiyo katika kuongeza uelewa wa vijana kuhusu dira na sera za chama.
“Tunakaribia uchaguzi mkuu, hivyo kampeni za kidijitali ni nyenzo isiyoepukika. Kupitia Kijani Ilani Chat Bot, vijana watapata fursa ya kujifunza na kuelewa zaidi dira ya chama chetu kuelekea uchaguzi,†alisema Mwinyi.
Aidha, Kawaida aliwataka vijana kuendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea Urais kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na mgombea mwenza wake Emmanuel Nchimbi, akiwapongeza kwa hatua ya kuchukua fomu za kugombea nafasi hizo.
Katika hotuba yake, alitoa pongezi kwa Katibu Mkuu mpya wa UVCCM Taifa, akimweleza kuwa ameandika historia ya kuwa kiongozi mdogo zaidi kushika wadhifa huo na kumhimiza kuhakikisha vijana wanatumia kikamilifu programu mpya ya Ilani ya Chama.
Akihitimisha hotuba yake, Kawaida alisisitiza vijana kupuuza upotoshaji wa mitandaoni unaohusiana na maandamano na badala yake wajikite katika maandalizi ya kushiriki uchaguzi mkuu wa Oktoba.
“Ni wajibu wa kila kijana kuhakikisha anajitokeza kupiga kura. Tuwape mkono Rais wetu na chama chetu kwa vitendo,†alisisitiza.
Mwisho, aliwashukuru vijana wote waliohudhuria hafla hiyo kwa mshikamano wao na mwamko wa kuunga mkono jitihada za chama kupitia nyanja za kidijitali. bofya hapa kutembelea https://kijanichatbot.or.tz/
Habari Zinazohusiana
TRILIONI 2.4 ZA RAIS DKT. SAMIA ZAAMSHA MUITIKIO MKUBWA KWA VIJANA WASOMI DAR ES SALAAM
23 Dec, 2025
Dar es Salaam, 23 Desemba 2025 Maelfu ya vijana wasomi wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar es Salaam wamejitokeza kwa wingi katika Hafla ya Ukaribisho wa Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza, iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC, chini ya Mgeni Rasmi Mwenyekiti wa UVCCM Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Ndg. Mohammed Ali Kawaida (MCC).
ATAKAYECHEZEA AMANI YA TAIFA LETU AWE ADUI YETU SOTE
21 Dec, 2025
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida, ametoa wito kwa vijana wote wa Kitanzania, viongozi na wananchi kwa ujumla kulinda, kutetea na kudumisha amani ya Taifa letu. Amesisitiza kuwa amani ya Tanzania ni tunu muhimu na ya msingi kwa ustawi wa Taifa, akibainisha kuwa yeyote atakayethubutu kuichezea amani hiyo hana nafasi katika jamii na anapaswa kuonekana kuwa adui wa wote.
Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Rais wa Tanzania
14 Dec, 2025
Dar es Salaam | 14 Disemba 2025 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Mheshimiwa Antonio Guterres, ameipongeza Tanzania kwa kuendelea kuwa kielelezo cha amani, mshikamano wa kijamii na utulivu wa kisiasa barani Afrika na duniani, licha ya changamoto zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.