BALOZI NCHIMBI AHUTUBIA WANANCHI ISAKA, SHINYANGA
04 Sep, 2025
32 Machapisho
Mgombea Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, leo amehutubia wananchi wa Isaka mkoani Shinyanga baada ya wananchi kumzuilia kwa shangwe kubwa akiwa njiani kuelekea Kagongwa kwa ajili ya Mkutano wa hadhara.
Katika hotuba yake, Balozi Nchimbi aliwaomba wananchi wa Isaka kumpa ridhaa Dkt. Samia Suluhu Hassan na wagombea wote wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, ili kazi kubwa ya maendeleo iliyoanza chini ya CCM iendelee kuimarisha maisha ya Waisaka na Watanzania kwa ujumla.
Wananchi wa Isaka kwa umoja wao wamesema wazi:
“Oktoba ni Samia – Mitano Tena kwa Maendeleo!”
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.