Balozi Dkt. Nchimbi Ahamasisha Wakazi wa Isaka Kuhakikisha Ushindi wa CCM Oktoba 29
04 Sep, 2025
86 Machapisho
Shinyanga, Septemba 3, 2025 – Mgombea Mwenza wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, leo Alhamisi amewahutubia maelfu ya wakazi wa mji mdogo wa Isaka, wilayani Kahama, Jimbo la Msalala, katika mkutano wa hadhara uliopambwa na hamasa kubwa za kisiasa.
Katika mkutano huo, Dkt. Nchimbi aliwanadi wagombea wa CCM kuanzia ngazi ya Ubunge hadi Udiwani, akimtaja kwa upekee Mabula Johnson Magangila, mgombea ubunge wa Jimbo la Msalala, pamoja na madiwani wa kata mbalimbali.
Akizungumza kwa msisitizo, Balozi Dkt. Nchimbi alisema kuwa anaendelea na ziara yake mkoani Shinyanga kwa lengo la kuinadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2025–2030, ambayo imejikita katika kuboresha maisha ya wananchi, kuongeza fursa za ajira, kukuza huduma za kijamii na kuhakikisha maendeleo endelevu katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Aidha, aliwaomba wananchi wa Shinyanga na Watanzania kwa ujumla kumpa kura za kishindo Mgombea Urais wa CCM, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na wabunge na madiwani wa chama hicho, ili kuhakikisha mwendelezo wa amani, utulivu, na maendeleo ya taifa.
“Mama Samia ni kiongozi mwenye dira ya maendeleo na anayo dhamira ya kweli ya kuwatumikia Watanzania wote. Kura zenu kwa CCM Oktoba 29 zitakuwa kura za kuendeleza ustawi na heshima ya nchi yetu,”
Mkutano huo umekuwa sehemu ya mwendelezo wa kampeni za CCM zinazofanyika nchi nzima kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.