MBALIZI HAINA JAMBO DOGO, YAFUNIKA MAPOKEZI YA DKT. SAMIA
04 Sep, 2025
60 Machapisho
Mbeya, Septemba 4, 2025 – Mapokezi ya kishindo yamemsubiri Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya maelfu ya wakazi wa Mbalizi kujitokeza kwa wingi kumpokea na kushiriki naye katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo.
Dkt. Samia ameanza ziara ya siku mbili mkoani Mbeya kwa lengo la kuinadi Ilani ya CCM 2025–2030, ilani ambayo imebeba majibu ya kero na changamoto za wananchi, ikiwemo kuboresha huduma za afya, elimu, miundombinu, kilimo na ajira kwa vijana.
Wananchi wa Mbalizi wameonesha hamasa ya hali ya juu, huku wakipaza sauti za ushindi na kuonesha imani kubwa kwa CCM na mgombea wao wa urais. Mkutano huo umekuwa ni ushahidi kwamba wananchi wa Mbeya wako tayari kumpa kura kwa kishindo ifikapo Oktoba 29, 2025.
Kwa mapokezi hayo ya leo, Mbalizi imeandika ukurasa mpya wa historia, ikionesha kwa vitendo kuwa “hawana jambo dogo mbele ya Dkt. Samia – ni ushindi wa kishindo pekee Oktoba 29.â€
📌 #OktobatunatikiFyuchaBilaStresi
📌 #KazinaUtutunasongaMbele
📌 #TunazimazoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo