MBALIZI HAINA JAMBO DOGO, YAFUNIKA MAPOKEZI YA DKT. SAMIA
04 Sep, 2025
14 Machapisho
Mbeya, Septemba 4, 2025 – Mapokezi ya kishindo yamemsubiri Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya maelfu ya wakazi wa Mbalizi kujitokeza kwa wingi kumpokea na kushiriki naye katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo.
Dkt. Samia ameanza ziara ya siku mbili mkoani Mbeya kwa lengo la kuinadi Ilani ya CCM 2025–2030, ilani ambayo imebeba majibu ya kero na changamoto za wananchi, ikiwemo kuboresha huduma za afya, elimu, miundombinu, kilimo na ajira kwa vijana.
Wananchi wa Mbalizi wameonesha hamasa ya hali ya juu, huku wakipaza sauti za ushindi na kuonesha imani kubwa kwa CCM na mgombea wao wa urais. Mkutano huo umekuwa ni ushahidi kwamba wananchi wa Mbeya wako tayari kumpa kura kwa kishindo ifikapo Oktoba 29, 2025.
Kwa mapokezi hayo ya leo, Mbalizi imeandika ukurasa mpya wa historia, ikionesha kwa vitendo kuwa “hawana jambo dogo mbele ya Dkt. Samia – ni ushindi wa kishindo pekee Oktoba 29.”
📌 #OktobatunatikiFyuchaBilaStresi
📌 #KazinaUtutunasongaMbele
📌 #TunazimazoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.