Dkt. Nchimbi: Utafiti Maeneo ya Madini Utaongezeka kwa 50%
05 Sep, 2025
86 Machapisho
Mgombea mwenza wa kiti cha Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesisitiza kuwa Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, endapo itapewa ridhaa ya kuingia madarakani tena, itahakikisha inatenga maeneo ya kutosha kwa Wachimbaji Wadogo wa Madini na kuongeza kiwango cha utafiti wa madini kutoka asilimia 16 hadi 50.
Kauli hiyo ilitolewa leo Ijumaa, Septemba 5, 2025, wakati Dkt. Nchimbi akiwa mkoani Geita, katika wilaya za Mbogwe na Nyang’hwale, huku akiendelea na mwendelezo wa mikutano ya kampeni za CCM kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.
"Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2025/2030 imedhamiria kuongeza tija kwenye sekta ya madini, kwa kutenga maeneo kwa Wachimbaji Wadogo. Vile vile, Serikali ya Dkt. Samia inakusudia kuongeza kiwango cha utafiti wa madini kutoka asilimia 16 hadi kufikia 50,"
Ongezeko la maeneo ya wachimbaji wadogo na kiwango cha utafiti wa madini litatoa fursa kubwa kwa vijana wa Tanzania, kwani watapata ajira za moja kwa moja kwenye sekta ya madini, ujuzi wa kisasa katika utafiti na usimamizi wa madini, na uwezekano wa kuanzisha biashara ndogo ndogo zinazohusiana na madini. Hii itasaidia vijana kuwa na kipato thabiti, kujitegemea, na kuchangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.
Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi anashirikiana na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakipeperusha bendera ya CCM, akisisitiza kuwa utekelezaji wa Ilani ya CCM ni sehemu ya kuhakikisha sekta ya madini inaleta tija, ajira, na maendeleo kwa wananchi wa Tanzania has Vijana
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo