DKT.ASANTENI SANA NJOMBE, NIMESHUHUDIA UPENDO NA MAPOKEZI MAKUBWA
05 Sep, 2025
26 Machapisho
Maelfu ya wananchi wa Njombe wamejitokeza kwa wingi kumpokea na kumsikiliza Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika mkutano wa kampeni uliofanyika mkoani humo.
Akihutubia wananchi, Dkt. Samia aliwashukuru kwa mapokezi makubwa na upendo waliomuonesha, akisema ni ishara ya imani kubwa waliyonayo kwa Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake.
Katika hotuba yake, aliwaeleza wananchi mambo mazuri ambayo Serikali ya awamu ya Sita imeyatekeleza mkoani Njombe kwa mwaka 2020 -2025 na mipango mizuri zaidi itakayotekelezwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa mwaka 2025-2030.
Aidha, aliwaomba wananchi waendelee kuamini na kuiunga mkono CCM, huku akisisitiza kuwa Oktoba 29 ni siku ya kufanya maamuzi ya kishindo kwa kutiki chama Cha Mapinduzi kuanzia Urais, Ubunge na Udiwani .
#OktobatunatikiFyuchaBilaStresi
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazimaZoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.